20/03/2025
Tumia karafuu,chumvi ya mawe na udi kutoa vifungo vya kichawi ama kusafisha nyota.
Chukua sufuria kubwa bandika maji yakuoga tia karafuu tembe 7 chukua udi kata vipande 7 chukua chumvi ya mawe tia katika maji uliyoweka kwenye sufuria lako.tia chumvi katika jiko/moto unaowaka tia vipande vyengine 7 vya udi katika jiko na tembe 7 za karafuu weka jikoni kisha sema maneno
Wewe ni sabuni ya utakaso naukatakase mwili,roho,nyota na maono yangu ya siku zijazo nauamuru uchawi na vifungo katika nyota vitoke na kupotelea katika sayari ya waovu niache nikiwa msafi na mwenye utakaso irudi nuru yangu na ubaki ukuu wangu iwe taa yakumlika na kuumbua wabaya katika uchawi mweusi ikasimame na kuwa kinga katika nuru yaende nayafanyike yale niyatakayo kwa mapenzi yangu.
kisha unalibandika sufuria la maji uliloweka vipande 7 vya udi tembe 7 za karafuu na chumvi ya mawe ndani yake yaache yachemke sana kisha tegua ukitamka haya
nakutegua uchawi,hila na laaana za watu wabaya nakugeuza na kukufanya ukawe tiba nakuitakasa nuru yangu.
weka kwenye ndoo ya maji nenda kaoge kwa kuyazunguusha maji yawe yanazunguuka duara ndio unachota unaoga hivyohivyo hadi yatapoisha ndani ya siku 7.
Na kabla yakufanya mambo haya uwe nauhakika ujakutana na mtu kimwili siku 7 zilizopita naufanye ndani ya hzo siku 7 na baada ya hapo ukae tena siku 7 yani siku 21 kamili usikutane na mtu kimwili 7 za mwanzo kujiandaa 7 za kati kutenda dawa na 7 za mwisho kukamilisha nguvu ya dawa